LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

12/23/09

Nyimbo za Injili zenye uvuvio wa nguvu ya Mungu zinauponyaji




Kheri ya Krismasi mpenzi msomaji wa blog hii, namshukuru Mungu kwa kutufikisha siku hii kwani wengi wameshindwa kufika baada ya kupoteza maisha yao kwa  njia ya ajali, ugonjwa na n.k.
Wiki hii aliyetawala katika safu hii ni Mtumishi wa Mungu  mwenye kipaji cha hali ya juu Kabula George  ambaye Mungu amekuwa akijidhihirisha kwa wanadamu kupitia nyimbo zake ambazo zimekuwa zikiwaponya watu waliofungwa na nguvu za giza kwa muda mrefu.
Kabula ambaye kwa sasa anatamba na albamu yake mpya ya Ushindi alisema kuwa, anamtukuza Mungu kwa kumtumia kadri awezavyo kwa sababu amekuwa akipata mialiko kutoka kila pembe ya nchi na awapo sehemu husika, Jehova hujidhihirisha kwa kuwaponya na kuwapa matumaini watu waliokata tamaa ya maisha na kuwaacha watu wakishindwa kuamini.
“Nina kila sababu za kumrudishia heshima na utukufu Mungu wangu kwa kujidhihirisha katika huduma yangu ambayo nimekuwa nikialikwa. Watu wengi wamekuwa wakipokea uponyaji pindi ninapokuwa naimba ama kuzisikiliza nyimbo zangu kwenye CD, kuziona kwenye VCD na DVD.
Hivi karibuni nilialikwa kwenye huduma moja jijini Dar es Salaam ijulikanayo kama Huduma ya Neno la Upatanisho (The Word of Reconciliation Ministries) na kupewa nafasi ya kuimba nyimbo mbili, kwanza niliimba  wimbo wa Hakuna Muweza ambao unasifu ukuu wa Mungu kisha nikamaliza na wimbo wa Dhihirisha ambapo nilimuomba Jehova adhihirishe uweza wake katika ya huduma hiyo.
Ghafla nguvu yenye upako wa aina yake ilishuka nikajikuta napiga magoti bila kutegemea na kuanza kububujikwa na machozi mara kila aliyekuwa kwenye huduma hiyo alishukiwa na nguvu hiyo na wote tukaanza kuomba.
Sikupata nguvu ya kunyanyuka, lakini Askofu wa Huduma hiyo Nicolaus Suguye ambaye naye alizama kwenye mambo, alipata alisimama na kuanza kuwaombea watu wenye shida mbalimbali. Siku hiyo taratibu zote za ibaada hazikufanyika, kwani askofu hakuhubiri tena kwa sababu watu walikuwa tayari wamezama kwenye maombi.
Baada ya huduma hiyo, mama mmoja aliyekuwa na uvimbe wa siku nyingi sehemu za siri alisimama na kushuhudia kuwa, wakati ninaimba ghafla alisikia nguvu inamshukia na kujikuta anaanguka chini bila kujitambua, na aliposimama uvimbe wote ulitoweka na sasa anaendelea na shughuli zake kama kawaida,” alisema Kabula.
Kabula alisema kuwa, anashuhuda nyingi sana ambazo amekuwa akipewa na watu wanaosikiliza nyimbo zake hasa wimbo wa Dhihirisha na Hakuna muweza ambazo zimeonekana kuwa tiba kwa watu waliofungwa na nguvu za giza.
Mtumishi huyo wa Mungu alisema kuwa, siri ya nyimbo zake kuwa tiba kwa watu wenye matatizo ni kutokana na nyimbo zake kuwa na uvuvio wa nguvu za Mungu ambazo watu wengi wametokea kuzipenda baada ya kubaini kuwa, hakuna haja ya kwenda kuombewa na askofu, mwinjilisti, ama mchungaji pindi wanapozisikiliza katika roho na kweli na kuyaweka kwa vitendo maneno yaliyomo ndani ya nyimbo hizo.
“Nyimbo zenye uvuvio wa nguvu ya Mungu zinauponyaji, namshukuru sana Mola kwa kuzivuvia nyimbo zangu nguvu yake, leo hii watu wanapata uponya, pasipo kwenda kuombewa katika mikutano ya dini ama makanisani,” alisema Kabula.
Kabula alimaliza kwa kusema kuwa; “Nyimbo zangu zinapatika kwa Mam Store atakayezihitaji kwa jumla na rejareja apige simu namba 0713328290, ama kama atanihitaji kwa ajili ya huduma awasiliane nami kwa simu namba 0757 140336.



The Holly Family Gospel Singers: Injili itolewe bure kwa ajili ya wote



KUNDI la muziki wa Injili la Makoma la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), limeendelea kuwa kundi bora la muziki wa Injili katika maeneo mbalimbali Afrika na duniani kote.

Kwa Tanzania yapo makundi mengi yanayofanya muziki wa aina hiyo likiwemo, J-Sisters, Rafiki Gospel Singers na mengine mengi ambayo kimsingi yanachangia kuongeza ukuaji wa muziki huo hapa nchini.

Lakini kwa hivi sasa mambo yanaonekana kuwa mazuri zaidi katika muziki huo baada ya Kundi la The Holly Family Gospel Singers kuonekana kuchomoza kwa kasi kwenye ulimwengu wa muziki huo huku likikubalika ndani na nje ya Tanzania kiwepesi.

Wakielezea mwenendo wao katika muziki wa Injili, waimbaji hao wanasema kuwa pamoja na kuwepo kwenye fani hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu sasa lakini bado wameendelea kukumbana na changamoto zilizopo kwenye fani hiyo kutokana na ukweli kwamba ni kazi ambayo inapigwa vita na shetani.

“Kazi hii si lelemama kuna majaribu mengi yanatukumba, ila tunamshukuru Mungu kwa kuwa ameendelea kutusimamia na kutupigania siku hadi siku kwani kama ingekuwa ni kwa nguvu zetu tusingeweza kufika popote,” anasema Ester Ntobi ambaye ni binti pekee kwenye kundi hilo lenye waimbaji watano.

Ntobi kwa niaba ya wenzake amefafanua kuwa, pamoja na changamoto zinazowakabili lakini wanamshukuru Mungu kuwapa kibali mbele za wanadamu kwani wamekubalika ndani na nje ya Tanzania, hii ni baada ya kupata mialiko mingi kwenye matamasha ya muziki huo.

Miongoni mwa mambo ambayo wanaona ni faraja kwao ni kupewa nafasi ya kufika katika maeneo mengi ambayo waimbaji wengi wamekuwa hawafiki au Injili imekuwa hasifiki mara kwa mara kutokana na mazingira au tamaduni za wanajamii husika.

“Kwa mfano, Zanzibar, Mafia na Mtwara ni maeneo ambayo tumekuwa tukienda mara kwa mara kwa ajili ya kufanya huduma ya kulitangaza Neno la Mungu, maeneo haya yamekuwa hayafikiwi na waimbaji wengi,” anafafanua Emmanuel Kapandila ambaye ni kiongozi wa kundi hilo.

Kadhalika siku chache zijazo wanatarajia kufanya ziara katika nchi za Uganda, Rwanda na Burundi, hii ni baada ya kupata maombi kutoka kwa makanisa ya Kikatoliki ya miji ya Jinja, Kampala, Kigali na Bujumbura na baadaye kwenda jijini Stockholm nchini Sweden na kisha mwakani wataelekea nchini Israel kwa ajili ya shughuli za hija katika miji mitakatifu ikiwemo mji wa Yerusalem.

Mbali ya mafanikio hayo, waimbaji wa kundi hili wanaeleza kwamba kuna mambo kadhaa ambayo wanaamini yanawakwamisha kwenye mikakati yao ya , hivyo serikali inatakiwa kuyaangalia kwa makini ili wanaovuja jasho waweze kunufaika na kile wanachokifanya.

“Ndugu yangu kwenye muziki wa Injili kuna matatizo mengi lakini tunachokiona hapa ambacho ni kilio cha watu wengi ni jinsi ambavyo kazi zetu zinavyoshindwa kutunufaisha, nadhani mimi nikiwa ni muinjilisti sitaki kutumia huduma hii kama biashara, lakini tunachohitaji ni kuhakikisha kazi yetu inawafikia watu wengi tena ikiwezekana bila malipo kwani hiyo ndiyo maana halisi ya Injili ya Yesu Kristo,” anaeleza Kelvin Hayola, ‘Black’.

Kundi hilo kwa sasa lina albamu moja iitwayo Nitakusifu yenye nyimbo nane, baadhi ya nyimbo hizo ni Nitakusifu, Bwana Unifadhili na Maombi Yangu zimeweza kulitangaza vema kundi hilo katika medani ya muziki wa Injili, ambalo kwa sasa lipo kambini likiandaa video ya albamu hiyo.

Rose Muhando, Mukubwa kunogesha tamasha krismasi




MWIMBAJI wa nyimbo za Injili raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), anayeishi Kenya, Solom Mukubwa na Malikia ya muziki huo nchini Rose Muhando wanatarajia kulinogesha  tamasha la Krismasi linalotarajiwa kufanyika ndani ya ukimbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Mbali na waimbaji hao ambao kwa sasa ndiyo wanaotikisa anga la muziki wa kumutukuza Mungu, watakuwepo pia Bahati Bukuku pamoja na Kundi la Upendo la Kijitonyama, Dar es Salaam ambalo mbali na kushiriki, wataadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa pamoja na kutambulisha albam yao, Jina Lako Li Hai, Upendo Nkone, na Flora Mbasha.

Siku hiyo pia Rose Muhando naye atatambulisha albamu yake ya Zawadi ya Krismas siku ya tamasha hilo iliyobeba nyimbo kama Amezaliwa Holini, Unaitwa Mbarikiwa, Nyota ya Ajabu, Hongera Kinamama, Anakuja Kwa Jina la Bwana na Eeh Bethelehemu.

Newer Posts Older Posts