LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

12/28/09

Nabii Josephat Mwingira wa Efatha Ministries


Mtume na Nabii Josephat Mwingira wa Efatha Ministries anayetikisa jijini la Dar es salaam na amejikusanyi waumini wengi kiasi kwamba huduma hiyo imepanua kwa muda mfupi.(Picha kwa hisani ya sayuni.blogspot)

Nabii Joedavie


Mheshimiwa Nabii Joedavie wa Ngurumo ya Upako anayetikisa jiji la Arusha, amejikusanyia maelfu ya watu kutokana na miujiza inayojitokeza kanisani hapo.(Picha kwa hisani ya sayuni.blogspot)

Westerwelle asema Ujerumani itasusia mkutano wa Afghanistan.

Berlin.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Guido Westerwelle, amesema kuwa atasusia mkutano wa kimataifa kuhusu Afghanistan, iwapo mkutano huo hautaangalia juhudi za ujenzi wa kiraia. Westerwelle ameliambia gazeti la kila wiki nchini Ujerumani la Stern kuwa iwapo mkutano huo utakaofanyika mwezi Januari mjini London utakuwa tu kuhusu kuchangia majeshi zaidi kwa ajili ya Afghanistan, Ujerumani haitashiriki. Hata hivyo, Westerwelle amerudia maelezo rasmi ya serikali kuwa itaangalia juu ya kuchangia waalimu zaidi kwa ajili ya jeshi la polisi . Kuongeza idadi ya wanajeshi wa Ujerumani nchini Afghanistan litakuwa si jambo linaloungwa mkono nchini humo.

EU yaitaka Israel kuangalia upya mradi wa nyumba.

Brussels.
Umoja wa Ulaya na Marekani zimepinga mipango ya Israel ya kujenga nyumba 700 katika eneo la Jerusalem ya mashariki. Katika taarifa, umoja wa Ulaya umeutaja ujenzi wa nyumba hizo kuwa ni kinyume na sheria chini ya sheria za kimataifa, wakati msemaji wa ikulu ya Marekani Robert Gibbs ameieleza mipango hiyo kuwa ni kitisho kwa amani ya eneo hilo. Wapalestina wanataka kulifanya eneo la Jerusalem ya mashariki kuwa mji wao mkuu wa taifa wanaloahidiwa na wanaungwa mkono na jumuiya ya kimataifa pamoja na umoja wa Ulaya. Israel wakati huo huo imesema mji wote wa Jerusalem ni mali ya taifa la Kiyahudi na imekataa miito ya kusitisha ujenzi wa makaazi katika eneo la mashariki inalolikalia.

Afghanistan kuchunguza shambulio la NATO.

Kabul.
Rais wa Afghanistan Hamid Karzai ameshutumu vikali shambulio la anga lililofanywa na majeshi ya NATO mashariki mwa nchi hiyo, ambalo linaripotiwa kuwa limesababisha vifo vya watu 10. Kwa mujibu wa maafisa katika ofisi ya rais, wanane kati ya wahanga walikuwa ni watoto wa shule. Msemaji wa bunge amesema kuwa tume itachunguza shambulio hilo. NATO inaripotiwa kuwa imekubali kushiriki katika uchunguzi huo.

30 wauwawa na bomu la kujitoa muhanga.

Karachi.
Mshambuliaji wa kujitoa muhanga ameshambulia mlolongo wa Waislamu wa madhehebu ya Kishia katika mji mkubwa nchini Pakistan wa Karachi na kuuwa watu 30. Kiasi watu 60 pia wamejeruhiwa. Watu walioshuhudia wamesema kuwa watu wawili ama watatu waliingia katika kundi la watu wapatao 50,000 waliokuwa wakishiriki katika maandamano ya Ashura na kulipua bomu lililokuwa limefungiwa mwilini. Mlipuko huo baadaye ulizusha ghasia mjini Karachi, mji wa kibiashara, ambapo watu wenye hasira walifanya ghasia. Lilikuwa ni shambulio la tatu dhidi ya sherehe hizo za Ashura nchini Pakistan mwaka huu. Siku ya Jumapili mshambuliaji wa kujitoa muhanga alishambulia msikiti wa Washia katika eneo linalomilikiwa na Pakistan la Kashmir na kuuwa watu saba. Bomu liliwajeruhi watu 17 mjini Karachi siku hiyo hiyo. Washia ni kiasi cha asilimia 20 ya jumla ya watu nchini Pakistan ambapo Wasunni ni wengi zaidi miongoni mwa watu milioni 167 nchini humo.

Muingereza kunyongwa China

Beijing.
Muda unakaribia kufikia mwisho kwa mtu mmoja raia wa Uingereza anayekabiliwa na hukumu ya kunyongwa nchini China. Akmal Shaikh mwenye umri wa miaka 53 alikamatwa Septemba 2007 mjini Urumqi magharibi mwa China akiwa na kilo nne za madawa ya kulevywa katika mzigo wake. Alihukumiwa kifo mwaka jana , Shaikh ameshindwa katika rufaa yake ya mwisho katika mahakama kuu mwezi huu. Waungaji wake mkono wanadai kuwa baba huyo mwenye watoto watatu ni mgonjwa wa akili, utetezi ambao hauna uzito wa kutosha kwa mujibu wa sheria za China. Hukumu ya kifo inatolewa kwa makosa kadha nchini humo na hutekelezwa mara zote. Mwaka jana kiasi cha zaidi ya watu 1,700 wamenyongwa.

Al Qaeda yadai kuhusika na jaribio lililoshindwa.

Washington.
Tawi la kimkoa la kundi la kigaidi la al-Qaeda, limetoa taarifa katika tovuti yake likidai kuhusika katika jaribio lililoshinda dhidi ya ndege ya abiria ya Marekani Desemba 25. Al Qaeda katika ghuba ya Arabia ama kama linavyojulikana kama AQAP, limesema kuwa mtuhumiwa, Umar Farouk Abdulmutallab alijaribu kuilipua ndege ya shirika la ndege la Northwest iliyokuwa imebeba watu 278 kulipiza kisasi kwa mashambulio ya majeshi ya Marekani dhidi ya kundi hilo nchini Yemen. Taarifa hiyo iliyotolewa katika tovuti kadha za Kiislamu imesema kuwa kundi hilo lilimpatia mtuhumiwa huyo wa Kinigeria mwenye umri wa miaka 23 kifaa kilichotengenezwa kwa ufundi wa hali ya juu, lakini kilishindwa kulipuka kutokana na matatizo ya kiufundi na kuwaonya Wamarekani kuwa watashambuliwa zaidi.

Westerwelle asema Ujerumani itasusia mkutano wa Afghanistan.

Berlin.

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Guido Westerwelle, amesema kuwa atasusia mkutano wa kimataifa kuhusu Afghanistan, iwapo mkutano huo hautaangalia juhudi za ujenzi wa kiraia. Westerwelle ameliambia gazeti la kila wiki nchini Ujerumani la Stern kuwa iwapo mkutano huo utakaofanyika mwezi Januari mjini London utakuwa tu kuhusu kuchangia majeshi zaidi kwa ajili ya Afghanistan, Ujerumani haitashiriki. Hata hivyo, Westerwelle amerudia maelezo rasmi ya serikali kuwa itaangalia juu ya kuchangia waalimu zaidi kwa ajili ya jeshi la polisi . Kuongeza idadi ya wanajeshi wa Ujerumani nchini Afghanistan litakuwa si jambo linaloungwa mkono nchini humo.

Newer Posts Older Posts