LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

01/07/10

Kipofu aanza kuona mara baada ya kusikiliza wimbo wa Dhihirisha


Nivigumu kuamini lakini ukweli ni huo kwamba, mtoto mmoja wa miaka 10, Anna Msingwa aliyezaliwa akiwa kipofu ameanza kuona huku Iringa, kwa mara ya kwanza baada ya wazazi wake kuusikiliza kwa kumanisha wimbo wa Dhihirisha wakiwa na mtoto wao ghafla nguvu ya mungu ilishuka na kujikuta wamezama katika maombi ya kumsihi Mungu amfungue macho kijana huyo, na walipomaliza kuomba mtoto wao walimuona anawaangali na kuanza kushangilia uponyaji.
Akiongea kwa njia ya simu na mratibu wa usambazaji wa albamu ya muziki wa injili ya Ushindi ya mwimbaji Kabula J.George, George Kayala kutokana Iringa, baba mzazi wa mtoto huyo, John Msingwa alisema kuwa, waliamua kuutumia wimbo huo kwa kumanisha kama muongozo wa maombi yao, baada ya kuusikiliza kwa muda mrefu na kubaini kwamba unanguvu zisizo za kawaida, waliamua kuweka wembo huo na kuanza kuabudu nao na walichokitarajia kikawa, na sasa mtoto wao anaona kama kawaida.
“Namshukuru Mungu kwa muujiza huu ambao amenifanyia kupitia wimbo huu, ni vigumu kaumini lakini ukweli unabaki palepale kwamba, mwanangu alikua haoni tangu kuzaliwa, tulipousikia wimbo wa Dhihirisha mimi na mke wangu tulimsihi Mungu ajidhihirishe kwa mwanetu aone kama wengine, na sasa anaona baada ya kuuimba kwa kumanisha wimbo huo,” alisema Msingwa.
Albamu hiyo inapatikana maduka yote ya kanda na kwa wamachinga nchini nzima, na kwa wale watakaoihitaji wawasiliane na mratibu wa idara ya usambazaji kwa namba 0755 240 136.

GIFT KALINGA AFUATA NYAYO ZA MWAITEGE


Msanii chipukizi wa  muziki wa Injili nchini Gift Kalinga,  amedai kuafuata nyayo za mzee wa ‘Utanitambuaji kama nimeokoka’ Bonny Mwaitege baada ya kuvutiwa na uimbaji wake ambao umempa  mafanikio  makubwa kimaisha na kihuduma.
Akichonga na safu hii  hivi karibuni, Kalinga alisema kuwa, tayari amekamilisha albamu yake ya kwanza yenye nyimbo nane na kuipa jina la Yesu anaweza, ambazo anaamini zitamtambulisha vema katika anga ya muziki huo kama ilivyo kwa Mwaitege ambaye amefanikiwa kujikusanyia mashabiki kila kona ya nchi.
“Napenda huduma ya uimbaji, lakini siwezi kuficha kuwa, nimelazimika kuingia studio na kufyatua albamu yangu hii baada ya kuvutiwa na uimbaji wa Mwaitege ambao kwa namna moja ama nyingine amefanikiwa kujikwamua kimasha kupitia huduma ya kumtumikia Mungu kwa njia hiyo,” alisema Kalinga.
Baadhi ya nyimbo zilizomo katika albam hiyo ni Yesu anaweza, Angalia, Niongoze Bwana na Jipe moyo ambazo zimekuwa zikichezwa  katika vituo vya radio za dini.




Newer Posts Older Posts