LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013
WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.
JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA
KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.
ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.
IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404
REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI
KIKOSI cha askari polisi wapatao 10, kimezusha hali ya wasi wasi katika maeneo ya Mwenge, jijini Dar es Salaam baada ya kujipangakatika eneo la karibu na Kanisa la Full Gospel Fellowship, ambalo wiki tano zilizopita, askofu wake, Zachary Kakobe alilitangaza kuwa la hatari kwa wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco).
Askofu Kakobe alitangaza hali hiyo baada ya Tanesco kutoa tamko la kutaka kupitisha njia ya umeme ya msongo mkubwa, mbele ya kanisa hilo licha ya waumini wake kupinga hatua hiyo kwa madai kuwa itaathiri mitambo ya kurekodi ibaada na kituo cha televisheni kinachotarajiwa kufunguliwa hivi karibuni.
Tangu wakati huo waumini wa kanisa hilo wameimarisha ulinzi nje ya kanisa hilo ili kuhakikisha kuwa mafundi wa Tanesco, hawaendelei na mpango wa kupitisha njia ya umeme ya kilovoti 132.Jana mchana baadhi ya wakazi wa Mwenge walipigwa na butwaa kuona askari wakiwemo watatu waliokuwa wamevalia sare huku wakiwa wamebeba bunduki na kujipanga umbali wa mita 10 kutoka kwenye eneo ambalo waumini wapatao 100, walikuwa wanalinda.
Waumini hao walikuwa wamevalia fulana za rangi ya njano na walikuwa wametulia katika eneo ambalo halina kivuli bila kujali jua, waliliambia Mwananchi kuwa wako tayari kupambana na askari hao.
Tukio hilo limekuja wiki mbili tu baada ya Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja kuzungumza na Askofu Kakobe kuhusu namna ya kumaliza mgogoro wa eneo hilo kwa njia ya amani.
Taarifa zililifikia gazeti hili jana zilisema askari hao walkwenda katika eneo hilo kwa lengo la kusimamia mafundi wa Kampuni ya Becco ambayo Tanesco imeipa kazi ya kutengeneza njia hiyo ya umeme.
Mafundi hao walikuwa wapime umbali uliopo kati ya Barabara ya Sam Nujoma na kanisa hilo lakini baada ya kuwasiliana na Askofu Kakobe, aliwakatalia kwa maelezo kuwa hawakumpa taarifa mapema.
Askari hao waliojipanga eneo hilo waliondoka saa saba mchana baada ya mafundi wa Kampuni ya Becco kutopata ridhaa ya askofu huyo ili kuendelea na kazi ya kupima eneo hilo.
Mwananchi lilipowasiliana na Kakobe, alisema wakati tukio hilo linatokea, alikuwa nje ya eneo la Mwenge kwa shughuli za kikanisa na alikataa kutoa ridhaa kwa sababu walipaswa kumuarifu mapema.
Alikiri kuwa kwenye mazungumzo yao na Wazairi, walikubaliana kupima umbali kati ya barabara na kanisa ili kujua athari za njia hiyo ya umeme lakini kilichomshangaza hawakutokea katika siku walizokubaliana.
Awali, Kakobe alisema kwamba Tanesco walilazimisha njia hiyo ipite upande wa barabara hiyo ambako kanisa lipo baada ya uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kuwakatalia kupitisha upande mwingine wa barabara hiyo.
HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuachia huru Mwenyekiti wa Chama Cha Demokratic (DP), mchungaji Christopher Mtikila, baada ya kukamilisha masharti ya dhamana katika kesi ya tuhuma za kupuuza kuhudhuria mahakamani.
Mchungaji huyo amekuwa mahabusu kwa zaidi ya wiki mbili zilizopita, kufuatia agizo la mahakama la kutaka akamatwe kwa kushindwa kuhudhuria kesi yake, inayohusu tuhuma za kumkashifu Rais Jakaya Kikwete.
Mapema wiki hii, wakili wake aliiomba mahakama impatie dhamana mteja wake.
Uamuzi wa mahakama kukubali ombi hilo, ulifikiwa jana na Hakimu Mkazi, Waliarwande Lema, baada ya kiongozi huyo wa DP, kukamilisha masharti ya kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja,alisaini bondi ya Sh1 milioni.
Pamoja na kutimiza masharti hayo, mchungaji Mtikila pia ametakiwa kusalimisha mahakamani, hati yake ya kusafiria na asitoke nje ya Jiji la Dar es Salaam, bila kibali.
Februari 8, mwaka huu atasomewa maelezo ya awali kuhusu kesi inayomkabili, hatua inayokuja baada ya upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi.
Januari 21, mwaka huu mchungaji Mtikila, kupitia wakili wake Mpale Mpoki, aliwasilisha ombi kwa mahakama kuiomba itengue uamuzi wa kumfutia dhamana.
Hata hivyo wakili wa serikali, Ponsiano Lukosi alilipinga ombi hilo kwa madai kuwa Mahakama ya Kisutu, haina uwezo wa kutengua uamuzi ambao ulikwishautoa.
Lukosi aliiambia mahakama hiyo kuwa kama upande wa utetezi unataka dhamana hiyo itenguliwe, basi inapaswa kwenda Mahakama Kuu ya Tanzania.
Akimfutia Mtikila katika kesi ya kashfa dhidi ya Rais Kikwete, hakimu Lema alisema mahakama imefikia uamuzi huyo kwa sababu hakuna sababu za msingi zilizokuwa zimetolewa na Mtikila juu ya kushindwa kuhudhuria mahakama.
Katika kesi hiyo inadaiwa kuwa Oktoba 21, mwaka jana katika maeneo ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Ilala, jijini Dar es Salaam Mtikila alitoa maneno ya uchochezi na ya dharau na kujenga chuki dhidi ya serikali na Rais.
HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuachia huru Mwenyekiti wa Chama Cha Demokratic (DP), mchungaji Christopher Mtikila, baada ya kukamilisha masharti ya dhamana katika kesi ya tuhuma za kupuuza kuhudhuria mahakamani.
Mchungaji huyo amekuwa mahabusu kwa zaidi ya wiki mbili zilizopita, kufuatia agizo la mahakama la kutaka akamatwe kwa kushindwa kuhudhuria kesi yake, inayohusu tuhuma za kumkashifu Rais Jakaya Kikwete.
Mapema wiki hii, wakili wake aliiomba mahakama impatie dhamana mteja wake.
Uamuzi wa mahakama kukubali ombi hilo, ulifikiwa jana na Hakimu Mkazi, Waliarwande Lema, baada ya kiongozi huyo wa DP, kukamilisha masharti ya kuwa na wadhamini wawili ambao kila mmoja,alisaini bondi ya Sh1 milioni.
Pamoja na kutimiza masharti hayo, mchungaji Mtikila pia ametakiwa kusalimisha mahakamani, hati yake ya kusafiria na asitoke nje ya Jiji la Dar es Salaam, bila kibali.
Februari 8, mwaka huu atasomewa maelezo ya awali kuhusu kesi inayomkabili, hatua inayokuja baada ya upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi.
Januari 21, mwaka huu mchungaji Mtikila, kupitia wakili wake Mpale Mpoki, aliwasilisha ombi kwa mahakama kuiomba itengue uamuzi wa kumfutia dhamana.
Hata hivyo wakili wa serikali, Ponsiano Lukosi alilipinga ombi hilo kwa madai kuwa Mahakama ya Kisutu, haina uwezo wa kutengua uamuzi ambao ulikwishautoa.
Lukosi aliiambia mahakama hiyo kuwa kama upande wa utetezi unataka dhamana hiyo itenguliwe, basi inapaswa kwenda Mahakama Kuu ya Tanzania.
Akimfutia Mtikila katika kesi ya kashfa dhidi ya Rais Kikwete, hakimu Lema alisema mahakama imefikia uamuzi huyo kwa sababu hakuna sababu za msingi zilizokuwa zimetolewa na Mtikila juu ya kushindwa kuhudhuria mahakama.
KAMA UNA HABARI NA MATUKIO MBALIMBALI POPOTE DUNIANI TUMA KWA EMAIL HII. productiongmk@gmail.com. NAMI NITAZIWEKA KWENYE BLOG HII BILA GHARAMA YOYOTE. NAKARIBISHA HABARI ZA MATAMASHA YA INJILI, MIKUTANO, RATIBA ZA MAKANISA, SEMINA, HARUSI NA MAMBO MBALIMBALI KWA AJILI YA KUWAJULISHA WANAULIMWENGU. WASILIANA NAMI KWA NAMBA ZIFUATAZO. +255 712 001 880, +255 755 240 136.