BONY MWAITEGE AZALIWA UPYA
Baada ya kukaa kimpya kwa muda mrefu bila kutoa albam mpya na kupelekea baadhi ya wadau wa muziki wa Injili kuhoji uwepo wa Bony Mwaitege katika huduma hiyo ya kumtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji, hatatimaye mwanamuziki huyo amewajibu waliofikiri amepotea baada ya kuibuka na albam mpya inayokwenda kwa jina la Mama. Albam hiyo kwa sasa imefanikiwa kuwateka watu wengi kutokana na vibao vyake kama Mama, na Njoo ufanyiwe maombi, Tega sikio, Inua macho, Omba msamaha, Maisha ni foleni, Ndio Bwana na Ni kwa neema.


