LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

KKKT lakemea mavazi ya kubana



KANISA la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kati, limekemea tabia iliyojengeka na  baadhi ya wanawake ya kuvaa mavazi ya kubana mwili ambayo yamekuwa chukizo kwa wanaume.(Pichani ni Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT nchini Dk Alex Malasusa)

Tamko hilo kali limetolewa na wanawake wapatao 234 wa kanisa hilo kwenye mkutano wao uliofanyika Usharika wa Manyoni, Jimbo la Kusini, mkoani Singida.

“Kanisa limesikitishwa juu ya mavazi yavaliwayo na wanawake kama vile suruali, mavazi ya mipasuo ya aibu na nguo za kubana, mavazi ya harusi yasiyoonyesha heshima na kwamba kwa kufuata msingi mavazi ya aina hiyo hayatakiwi kuvaliwa kanisani na mwanamke au mwanaume,” lilifafanua tamko la wanawake hao.

Kwa mujibu wa tamko hilo, mwanamke ametakiwa asivae mavazi yamfaayo mwanaume wala mwanaume naye asivae mavazi ya mwanamke kwa maana kwamba kila afanyaye hayo humchukiza Mungu.

Katika kilele cha sikukuu hiyo ya wanawake, pia kulifanyika harambee ya kuchangia matengenezo ya gari pamoja na ununuzi wa kompyuta, ambapo jumla ya sh 2,177,810 zilikusanywa na kwamba kati ya hizo sh 1,177,000 ni ahadi na fedha taslimu ni sh 404,810.

Wakati huo huo, usharika wa Tabata Kuu umemuomba mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Alex Malasusa kutoa tamko la wazi kupinga uamuzi wa kanisa hilo nchini Marekani na Ulaya kuruhusu ndoa za mashoga.

Ombi hilo lilitolewa mwishoni mwa wiki na Mchungaji Erasto Ailla wa usharika huo wa KKKT alipohubiri kwenye maadhimisho ya siku kuu ya Krismasi ya kuadhimisha miaka 2009 ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. Mchungaji huyo pia aliongoza sala maalum ya kupinga vitendo hivyo.

Mchungaji Ailla, akionyesha kusikitishwa na vitendo hivyo kwa makanisa ya nchi za Magharibi, alisema taarifa za kanisa hilo nchini Marekani na barani Ulaya kubariki ndoa za mashoga na wengine kuongoza ni kumkejeli Mungu ambaye ametamka wazi kwamba waovu wa aina hiyo hawatauona ufalme wa Mungu.

Alimuomba Dk Malasusa tamko la kupinga uamuzi huo kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla na kwamba yeye anaamini kwamba kanisa hilo barani Afrika halitakubali kuruhusu mashoga kuoana kwani ni kinyume na maagizo ya Mungu.

"Kwa kuanzia, nawaomba waumini wote usharika huu tuwe wa kwanza kupinga na sasa tusimame, tufumbe macho na kuomba sala maalum ya kukataa ushoga ndani ya kanisa na kukiri wazi kwamba mashoga... wanamchukiza Mungu kama wale wa Sodoma na Gomola," alisisitiza na kuwaongoza waumini kwa sala maalumu ambayo pamoja na mambo mengine pia ilikuwa inakataa ushoga kwa mbinu zote.

Kanisa la Kilutheri nchini Marekani liliruhusu ndoa za mashoga baada ya uamuzi huo kupitishwa kwenye mkutano wake mkuu, na kuwa kanisa la pili baada ya Anglican ambalo pia ni la Marekani.




Newer Post Older Post