Mwimbaji wa muziki wa Injili nchini Rose Muhando amepata pigo baada ya kufiwa na dada yake Salma Muhando usiku wa kuamkia leo na msiba uko nyumbani wako Tanga, Kilindi. Wadau wote wa Rose tuko naye katika hali hii ya majonzi na Mungu ailaze mahala pema pepo roho ya marehemu, kwani Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe Amen.
TZ GOSPEL MUSIC
Thursday, October 13, 2011
Rose Muhando apata pigo
Mwimbaji wa muziki wa Injili nchini Rose Muhando amepata pigo baada ya kufiwa na dada yake Salma Muhando usiku wa kuamkia leo na msiba uko nyumbani wako Tanga, Kilindi. Wadau wote wa Rose tuko naye katika hali hii ya majonzi na Mungu ailaze mahala pema pepo roho ya marehemu, kwani Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe Amen.
Tuesday, August 16, 2011
RADIO USHINDI FM
SEMINA YA MWALIMU MWAKASEGE
Semina hiyo itakuwa inaanza saa 9 alasiri mpaka saa 12 jioni kila siku. Semina hiyo imeandaliwa na Kamati ya Maandalizi ya Mwl.Christopher na Diana Mwakasege, watu wote mnakaribishwa. Picha kwa hisani ya Amani masue bloG
Saturday, July 30, 2011
J. SISTERS KUZINDUA ALBUM CHUKUA USHINDI
Friday, July 29, 2011
HAKIGRAM IKITUMIKA IPASAVYO ITAWANUFAISHA WASANII
Naungana na serikali kupitia Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adam Malima kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, alipokuwa anajibu swali Mbunge wa Viti Maalum, Esther Bulaya (CCM) mjini Dodoma Julai 27, 2011.
Ni ukweli kwamba, utaratibu wa kila msambazaji kuingia mkataba na msanii kusambaza idadi flani ya nakala na kupewa stika za HAKIGRAM ambazo zitabandikwa kwa kila nakala kutawezesha kujua msanii kauza nakala ngapi na kwa muda upi.
Kazi nyingi za wasanii wa Tanzania zinauzwa kinyume na sheria nchi za Congo , Burundi , Malawi , Rwanda na Zambia .
Waharamia wa kudurufu kazi za wasanii wametajirika huku wahusika wakiwa katika hali ya umasikini na wanafanya bila uoga kutokana na kosekana kwa sheria ya kuwabana moja kwa moja.
Nasema hivyo nikiwa na ushahidi kuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Auction Mart, Alex Msama ambaye amekuwa akipambana na maharamia hawa kila kukicha.
Hivi karibuni Msama alifanikiwa kukamata mtambo mmoja mkubwa wa kudurufu CD wenyewe uwezo wa kuzalisha CD feki 300 ndani ya dakika 20.
Na ili zoezi hili lifanikiwe inatupasa waimbaji wote wa muziki wa Injili na wadunia kuungana kwa pamoja ili kuondoa ujangili huu ambao unadidimiza maisha ya wasanii huku wasiohusika wakitajirika.
Mpaka sasa Msama amefanikiwa kuwakamata baadhi ya wanyonyaji kama Fred Jumbe, Martin Mkinga na Mstafa Rashidi.
Thursday, July 21, 2011
VIONGOZI WA DINI NA MADAWA YA KULEVYA
Ni Mungu yupi wanayemtumikia viongozi hawa wa dini wanaojihusishwa na madawa ya kulevya?
Monday, July 18, 2011
MWINJILISTI WA KIMATAIFA KABULA GEORGE AWAPONGEZA WAKENYA
Mwinjilisti wa kimataifa Kabula J.George amewapongeza wananchi wa Kenya hasa mkoa wa Kisii kwa mapokezi yao mazuri waliyompa kwenye kanisa la Mlima wa Sayuni na kumwandalia mkutano mkubwa wa nje ulioponya watu wengi. Kabula amewashukuru waumini wa kanisa hilo kwa ukarimu wao wote waliouonesha kwa muda wa wiki moja akiwa kanisani hapo kwa ajili ya kulihubiri neno la Mungu kwa njia ya uimbaji na kuhubiri.
Anashukuru Mungu pia kutumia wachungaji wote wa kanisa hilo pamoja na Edward Makoli. Kabula alitumia nafasi hiyo kuwakaribisha waumini hao kuja Tanzania kwa ajili ya kulitangaza neno la Mungu.
Sunday, July 17, 2011
SEMINA YA MASOMO YA NDOA
Kwa mialiko ya semina za ndoa piga simu namba +255755240136 ama +255656215572.
Subscribe to:
Posts (Atom)









