LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

KWA NINI WATU WENGI HAWAJIBIWI MAOMBI YAO? - 2

Apostle George Kayala

Namshukuru Mungu kwa kutuamsha salama tena siku ya leo kwani kuna wengi walitamani kuiona siku ya leo lakini hatuku nao. Si kwamba mimi na wewe ni watakatifu sana kiasi kwamba tuwe wazima mpaka sasa bali ni neema yake Mungu aliyotupa tena leo. Nimaombi yangu hata sasa unaposoma somo hili jitahidi kuwa katika hali ya toba wakati wote kwani hujui sekundi moja ijayo nini kitatokea katika maisha yako. Mimi na wewe hatujui ni nani anayeweza kutwaliwa siku ya leo. Tambua hakuna mtu anayejua siku yake ya kufa. Watu wengi hujua mipango yao ya maisha na kujiwekea malengo ya muda mfupi na mrefu wakiwa na uhakika wakufika huko.


Swali waliotangulia jana na usiku wa kuamkia leo ina maana hawakuwa na malengo? Jibu ni kwamba nao walikuwa na malengo kama wewe ila hawakujua siku yao ya kufa na waliamini kabisa kuwa watatimiza malengo yao. Ni maombi yangu malengo yako uyaweke mkononi mwa Bwana ili akufanikishe hata kama atakuchukua leo utakuwa na faida ya kuishi naye milele.
Ame, ngoja tuendelee na somo letu la KWA NINI WATU WENGI HAWAJIBIWI MAOMBI YAO? Jana nilimaliza kwa kusema kuwa kila unaloomba Mungu anauwezo nalo na haakuna la kumshinda. Mandiko katika kitabu cha Yeremia 32:27 yanasema “Tazama mimi ni BWANA Mungu wa wote wenye mwili  je! Kuna neno gumu lolote nisiloliweza?.
Kumbuka kuwa Mungu ndiye ampaye kila mtu ampendaye. Swali la kujiuliza ni kweli wewe hakupendi mpaka asisikie maombi yako? Kitabu cha  Danieli 4:25, 34 maandiko yanasema kuwa; "Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu naye humpa yeye amtakaye, awaye yote . . . mamlaka yake ni mamlaka ya milele, na ufalme wake hudumu toka kizazi hata kizazi."
Ukitaka Mungu akujibu kwa haraka maombi yako, hakikisha unapoingia kwenye maombi uwe umeshajitakasa na kusamehe wale waliokukosea. Lakini wakati mwingine wewe ndiye unayesababisha Mungu achelewe kujibu maombi yako kwa sababu unaingia kwenye maombi ukiwa katika chuki na waliokukosea.
Maandiko yanasema kuwa Tunajua ya kuwa Mungu hawasikilizi wenye dhambi, lakini huwasikiliza wote wanaomcha na kumtii.” Yohana 9:31. Kama utakuwa na kawaida ya kuingia katika maombi huku ukiwa na fundo la dhambi ya kutowasamehe waliokukosea na kujitakasa, hakika utaomba na kufunga mpaka unapata vidonda vya tumbo na hutapata hitaji la moyo wako.
Maandiko yanaendelea kusema kuwa Vumilianeni na kusameheana. Mtu akiwa na lalamiko lo lote dhidi ya mwenzake, sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi. Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika amani kamilifu,” Wakolosai 3:13-14. Katika maandiko haya Mungu anatoa amri ya kumsamehe kila mmoja. Hii inamaanisha kwamba kama unataka kusamehewa dhambi zako lazima kusamehe wale ambao wamekukosea au wametenda  dhambi juu yako.
Na kama hiyo haitoshi Mungu anakutaka usamehe hata kama unakosewa mara kwa mara. Mathew 18: 21-22;  Ndipo Petro akamjia Yesu na kumwuliza, “Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi nami nimsamehe? Je, hata mara saba?” Yesu akamjibu, ‘‘Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.’’
Kwa leo naishia hapa nakusihi endelea kufuatilia somo hilo naamini litakusaidia.
Naitwa Apostle George Kayala
Kwa maoni na ushauri niandikie kwa barua pepe; gmkproduction77@gmail.com

Newer Post Older Post