LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

KWA NINI WATU WENGI HAWAJIBIWI MAOMBI YAO?

Apostle George Kayala
Wapendwa katika Bwana, nimesukumwa moyoni kuwa natoa masomo ya biblia kwa njia hii ikiwa ni moja ya kukumbushana juu ya safari yetu ya kuelekea mbiguni. Katika somo letu la leo tutaangalia kwa nini watu wengi hasa waliookoka huwa hawajibiwi maombi yao kama wanavyoomba? Kama ni bidii ya maombi wanafanya lakini haja ya maombi yao haitekelezeki. Wakati mwingine mpaka wanafikiri kuwa Mungu hasikii maombi yao na kujikuta muda mwingi wanabaki kunung’unika. Watu wengi hawajui kuwa kushindwa kujibiwa kwa maombi yao kunatokana na jinsi wanavyoomba.
Wapo wanaoomba ili wananikiwe wapate kuwatishia wenzao, ama kutumia kinyume na mapenzi ya Mungu kile anachoomba. Unaweza kukuta mtu anasema mimi naomba Mungu anipe pesa kwa ajili ya huduma yake lakini kumbe moyoni mipango iko tofauti.
Kaka wewe ni miongoni mwa watu ambao wameomba muda mrefu bika kupata haja ya kile unachoomba soka kitabu hiki. Yakobo 4:3 “Hata mwaomba walahampati kwa sababu mwaomba vibaya ili mvitumie kwa tamaa zenu”.
Ili Mungu akujibu kile unachoomba inakupasa kuomba sawasawa na mapenzi yake na siyo yako. Kumbu kuwa Mungu ni Roho, hivyo huwezi kumdanganya kwa lolote katika maombi yako ambayo naweza kuyaita ni ya ubabaishaji.
Katika kitabu cha 1Yohana 5:14-15 biblia inasema Na huu ndio ujasiri tulionao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. 15 Na tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba .
Naamini mpaka hapo utakuwa umejifunza kitu fulani kwa haya machache niliyokweleza. Nitaendelea na somo hili kesho naomba usikose kulifuatilia kwani ni imani yangu mpaka mwisho wa somo utakuwa umejifunza kitu na utabadili mwenendo wa maombi yako.
Elewa kuwa kila unaloomba Mungu anauwezo nalo na haakuna la kumshinda. Mandiko katika kitabu cha Yeremia 32:27 yanasema “Tazama mimi ni BWANA Mungu wa wote wenye mwili  je! Kuna neno gumu lolote nisiloliweza?.Sikiliza msomaji mpendwa Hakuna jambo gumu la Kumshinda Bwana.

Naitwa Apostle George Kayala
Kwa maoni na ushauri niandikie kwa barua pepe gmkproduction77@gmail.com

Newer Post Older Post