LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

Peter Baguma: Aweka Bongo Flava pembeni ili amtumikie Bwana


 PETER Baguma ni mwanamuziki wa injili aliyeamua kumrudia Mungu kwa kuamua kuachana na muziki wa Bongo Fleva aliokua akiuimba na kubadili mtazamo wake na kuanza kumuimbia Mungu kuanzia mwaka 2004.
Kama ilivyo kwa waimbaji wengi, Baguma alianzia kuonesha kipaji chake cha uimbaji kanisani, kutokana na uimbaji wake uongozi wa kanisa ulimchagua kuwa kiongozi wa kwaya iliyojulikana kwa jina la Team of Mission.
Alipojitoa kwenye kundi hilo alilodumu nalo kwa miezi nane kabla ya kusambaratika, aliamua kujitosa rasmi kwenye uimbaji wa kujitegemea akiwa na lengo la kuwasaidia watu wa hali ya chini.
 Anaeleza kuwa katika albamu yake ya kwanza ambayo inajulikana kwa jina la Yesu Nuru Yangu, aliwashirikisha vijana mbalimbali wanaoishi kwenye mazingira magumu.
“Niliwasaka mitaani na kuimba nao ili kuona wenye vipaji kisha nikawachukua na kufanya nao kazi, walijisikia amani na wengi wameonyeshwa kufurahia tendo hilo,” anasema Baguma.
Akielezea ugumu anaokutana nao kwenye kazi hiyo ni vitendo vya ‘maprodyuza’ kuweka kipaumbele fedha kuliko kazi, hali inayochangia kuwakatisha tamaa waimbaji walio wengi.
Anafafanua kuwa kuna baadhi ya wadau wameugeuza muziki huo kuwa biashara, hivyo kushindwa kufanya katika ufanisi unaotakiwa kutokana na kuiga vipaji vya watu wengine na kuacha vipaji vyao halisia vikipotea.
Kitu cha msingi kinachotakiwa ni mtu kujitahidi kutoka katika hali halisi aliyo nayo na kujiboresha zaidi kwa kutoiga kwa mtu mwingine ili kuuboresha zaidi muziki wa Injili kuweza kuwa na ladha tofauti zitakazosaidia kuuweka juu siku zote.
 “Ili kuuendeleza muziki wa Injili hapa nchini ni vyema waimbaji wanaochipukia wajaribu kuwa wabunifu katika kazi zao na wawe wepesi kujifunza kutoka kwa wanaojua pindi wanapoambiwa kwa ajili ya maboresho na kuwa na msimamo wa hali ya juu katika maamuzi yao.
“Kuna wanamuziki wenye majina makubwa wamekuwa na wivu wa kutotaka kutoa ushirikiano kwa chipukizi kwa kuwapa msaada, ili waweze kufanya vizuri zaidi kitu ambacho kinarudisha nyuma maendeleo ya muziki wa Injili nchini.
“Wivu usio na faida hauwezi kutufikisha mbali ni vema waimbaji wakaondokana na tabia ya ubinafsi katika kumuimbia Mungu ili kuweza kupiga hatua zaidi kwa kutomdharau mtu yeyote na ukweli kwamba wivu unasababisha matatizo kwenye milango ya mbele,” anasema Baguma.
Anamalizia kwa kusema kuwa ili fani yao izidi kupiga hatua, vijana wanaochipukia wasikate tamaa katika kuimba, wajitume ili wasonge mbele na kuangalia kile wanachotaka kufanya kiwe na msukumo wa hali ya juu pamoja na kuwa na imani katika kazi.

Newer Post Older Post