LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

Pastor Wambura - Sijaukana ulokole

Mwanamuziki wa muziki wa Injili nchini Steven Wambura, ambae ilidaiwa alikuwa akitaka kuingia katika muziki wa kidunia ameibuka upya na kukanusha vikali madai hayo.
Akiongea na safu hii Wambura alisema kuwa wakati yuko Moani Arusha ambako ndio makazi yake alisikia wapinzani wake wakisema maneno hayo na kudai ameishiwa kabisa na amejiunga na bendi ya Tanzanite iliyoko huko hivyo kumuasi bwana.

“Siwezi katu kuimba muziki huo na kama nitashindwa kabisa basi nitabaki kumuimbia bwana kanisani kwani ninaimani ujumbe utafika na sio kuingia katika bendi za kidunia,” alisema.
Hata hivyo aliongeza kuwa anashangazwa na maneno hayo ya waimba injili chipukizi ambao anahisi walikuwa wanataka kumchafulia ili aonekane ni kondoo aliyepotea kitu ambacho si kwani hivi sasa amesha kamilisha Album yake mpya iitwayo Roho wa Bwana na inaendelea kufanya vizuri katika television na redio mbalimbali nchini.

Wambura, ambaye sasa anatamba na kibao chake cha 'Roho wa Bwana' amesema baadhi ya wanamuziki wa Injili wanashangaza kwa tabia hizo lakini yeye anaamini hiyo ni dalili ya kufika kwa siku za mwisho.

Katika hatua nyingine Wambura amedai kuchukizwa na waimbaji wa muziki huo ambao wamekuwa wakipata kiburi kila kunapokucha kutokana na kupata majina makubwa katika jamii inayowazunguka na kujiona wao ni bora kuliko wengine.

Wambura alisema kuwa, leo hii si jambo la ajabu kuona baadhi ya wanamuziki wa muziki huo wakipata kiburi, maringo na dharau baada ya kufanikiwa badala ya kuendelea kutoa huduma ya kiroho kwa mapana na marefu na baadhi yao hawajasimama katika huduma ya uimbaji.

Aliendelea kudai kuwa kipindi waimbaji hawa wakiwa hawajainuliwa,  hushinda kanisani wakisali na kuomba na wakati mwingine kuhitaji misaada kwa watu ili watoke katika hatua moja kwenda nyingine, lakini baada ya mafanikio huwadharau hata watu ambao waliwasaidia katika siku za awali.

Mtumishi huyo wa Mungu aliendelea kusema kuwa, baadhi ya waimbaji wamekuwa wakiimba kwa ajili ya kutafuta fedha zaidi kuliko kumtumikia Mungu wao ambaye ndiye anawawezesha kufikia mafanikio wanayoyafikia.

Mwanamuziki huyo anasema ni kweli mtu hufanya kazi ya muziki wa Injili akiwa na lengo la kufikisha ujumbe wa Mungu kwa mataifa na mwisho wa siku anahitaji kujikimu katika maisha ya kawaida. Na hayo yanaweza kutimia kama mtu akiwa na fedha.

"Pamoja na kwamba tunahitaji fedha za kujikimu si sahihi kuzitafuta kwa njia za ajabu na kusahau kuwa lengo letu ni kutoa huduma na fedha zinakuja baadaye.

"Kwa kawaida hakuna kiwango cha fedha ambacho mtu anaweza kukitaja kwa ajili ya kutoa huduma ya Mungu, lakini unapojitoa katika kazi hiyo hata Mungu anakubariki na mambo mengine yanakunyookea.

Nyimbo zinazopatikana katika hiyo mpya inayokwenda kwa jina la 'Roho wa Bwana', ambao ni 'Amtegemeae Mwanadamu', 'Usiipende Dunia', Yesu Amesikia Kilio Chako', 'Mwache Yesu Atawale', 'Upendo', 'Hakuna Kama Wewe' na 'Kuja Kwa Yesu'.

Wambura, ambaye alianza kuimba tangu akiwa mdogo katika Kanisa la TAG, Kijenge, Arusha amesema anafurahia mafanikio aliyoyapata kwani sasa anafahamika na muziki wake unakubalika kwa watu wa rika zote.

"Napenda kuona watu wa rika zote wakimtukuza Mungu, napoona kazi yangu inasonga mbele namshukuru sana Mungu wangu ambaye ndiye anayeniwezesha kupiga hatua kila kukicha."

Akielezea suala la kuzungumza kwa lafudhi kama ya watu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Wambura alisema kuwa watu wengi wanafikiri anatoka katika nchi hiyo lakini yeye ni Mtanzania, bali muda mrefu ameishi na watu wa Kongo.

"Nilipata lafudhi ya Congo kutokana na kuwa karibu mno na watu wa nchi hiyo. Mwaka 1999, nikuwa Afrika Kusini, ambapo nilikuwa nikifundisha muziki katika Chuo cha Muziki cha Amakosi Theatre jijini Johannesburg, huko nilikuwa na rafiki wengi kutoka Congo . Suala la kuwa nao karibu kwa miaka mingi, limenifanya nizungumze kama wao," anasema Wambura ambaye ni mume wa Penita na baba wa mtoto mmoja aitwaye Timoth.

Newer Post Older Post