LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

Kilaini awaanga wakazi wa Dar


Aliyekuwa askofu Mkuu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki la Dar es Salaam, Methodius Kilaini, ambaye amehamishiwa Jimbo la Bukoba, amewaaga rasmi waumini wa Jimbo hilo na kudai kuwa atawakumbuka kwa upendo wao waliokuwa nao juu yake(Picha kwa hisani ya Habari Leo).

Akiwaaga waumini hao kupitia ibada ya Misa ya sikukuu ya Krismasi iliyofanyika kwenye Kanisa la Mtakatifu Joseph, Kilaini alisema kuwa, mbali na kuwakumbuka, pia amewataka Watanzania wote kuliombea taifa lao ili uchaguzi mkuu wa mwakani uwe wa amani na utulivu.

Kilaini alisema kuwa, Watanzania wana wajibu wa kuwaombea viongozi wa vyama vya siasa ili washiriki katika uchaguzi huo bila kuvunja amani.

“Kama tunavyojua, mwaka kesho tuna uchaguzi, katika nchi yoyote uchaguzi ni kitu cha muhimu, tumwombe Mwenyezi Mungu uchaguzi uwe wa amani , tuwaombee wenyeviti wa vyama vya siasa ili watupitishe mwaka ujao salama na tupate viongozi watakaotufikisha miaka mitano ijayo salama,” alisema Kilaini.

Katika hatua nyingine Kilaini alitumia nafasi hiyo kuwasamehe watu wote mabaya waliyomfanyia wakati akiwa Askofu Msaidizi wa jimbo kwani ni hali ya kibinadamu na hivyo hana budi kuyasahau na pia waumini wa kanisa hilo walitumia misa hiyo kumuaga rasmi.

Newer Post Older Post