LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

Alex Msama: SIMWACHI ROSE


Bosi wa kampuni ya Msama Promotion, Alex Msama Mwita, amekanusha kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injili nchini, Rose Muhando.
Msama alifikia hatua hiyo ikiwa ni saa chache toka kuingia mtandao kwa habari hii iliyoandika kuwa; ROSE MUHANDO AIPASUA NDOA YA MTU.
Mkurugenzi huyo alisema kuwa, toka habari hiyo isomeke kwa wadau wengi, amekuwa akipigiwa  simu za kumpa pole kwa tukio hilo.(Msama kushoto akifafanua jambo ndani ya ofisi ya TGM)
“Hii habari imenipa wakati mgumu sana, kila mtu pole, pole, mpaka nimekatisha usingizi leo. Mmi sikubali, nataka kujua aliyewaletea nyinyi hizi habari. Unajua hata Meneja wa Rose (Muhando), Nathan naye amenipigia, kaniuliza nani anayeleta habari mtandaoni?” Alisema Msama.
“Mimi na Rose tuko karibu sana, lakini kikazi na siwezi kumwacha, nimetoka naye mbali. Nimefanya naye matamasha mengi mengi, hata hivi karibuni tutafanya jingine la Pasaka,” alisema Msama.

Aliongeza kuwa, kama kuna wanaofikiria vibaya kuhusu ukaribu wake na Rose, “basi wanakosea sana, ni kwa ajili ya kazi tu na kwa hilo mimi siwezi kumwacha Rose kwa sababu hatuna kitu kingine kibaya baina yetu na tunaheshimiana sana,” alisema Msama.
Akipangua zaidi ishu hiyo, Msama alisema kuwa, yeye, mkewe, Rose na meneja wa Rose, Nathan wanamtafuta ‘mchawi’ anayewawangia usiku na mchana na kusababisha pole zisizokuwa na sababu.

Newer Post Older Post

One Response to “Alex Msama: SIMWACHI ROSE”

Limbe Juma said...

Umaarufu jalala. Hata iweje watu wataendelea kusema na kuzusha mambo na huo ndio ukweli wenyewe wa maisha hapa duniani. Hata ukifa napo utasemwa tu! Walimsema na kumzushia mambo Yesu Kristo sembuse Rose Muhando?

Ni vizuri kukanusha lakini wakati mwingine ni vizuri pia kuyaacha mambo hayo yakajifia yenyewe. Cha muhimu ni kumtegemea Mungu na kujikabidhi kwa Mungu kwa nia ya kweli. Mengine yote ni madogo.

Poleni sana kwa changamoto hii. Mungu Awe nanyi daima!