LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

PASAKA NI NINI?

Pasaka ya Kiyahudi ni kati ya sikukuu muhimu zaidi za dini ya Uyahudi. Sikukuu hii inakumbuka kutoka kwa Wanaisraeli kutoka utumwa walimokuwemo huko Misri.

Pasaka ya Kiyahudi imekuwa na athira kubwa juu ya sherehe ya Pasaka ya Kikristo kuhusu tarehe, liturgia na desturi mbalimbali.

Jina la Pasaka limetokana na neno la Kiebrania "פסח" (tamka: pasakh) lenye maana ya "kupita juu, kukaa juu ya (kama mlinzi)" katika kitabu cha Biblia cha Kutoka 12:23. Hapa imeandikwa ya kwamba Mungu "atapita" juu ya milango ya nyumba za Wanaisraeli huko Misri katika usiku kabla ya kutoka kwao, na kuzuia maovu ambayo Wamisri waliathiriwa nayo.
Meza ya Seder yaani Chakula cha Pasaka ya Kiyahudi ikionyesha vitabu vya Haggada
Sahani ya Seder ya Pasaka ya Kiyahudi

Pasaka ina tarehe kamili katika kalenda ya kiyahudi inaanza Nisan 15. Husheherekewa kwa siku saba yaani hadi Nissan 22. Siku ya kwanza na ya mwisho ni sikukuu hasa. Katika nchi ya Israel siku hizi mbili ni siku za kupumzika kazi. Wayahudi wengine hasa nje ya Israel husheherekea siku 8.

Kwa sababu kalenda ya kiyahudi ni kalenda ya mwezi tarehe zake hubadilika katika hesabu ya kalenda ya Grigori yaani kalenda ya kawaida ya kimataifa. Kwa jumla Pasaka ya Kiyahudi inasheherekewa wakati wa miezi Machi au Aprili kwa sababu Nisan ni mwezi wa majira ya kuchipua.

Asili ya Pasaka

Katika Biblia, kitabu cha Kutoka, sura ya 12, kuna taarifa ya kutoka kwa Wayahudi katika Misri wakati wa Musa mnamo mwaka 1200 KK. Taarifa ni ya kwamba Musa alitumwa na Mungu kuwaondoa Wanaisraeli katika hali ya utumwa huko Misri na kuwaongoza kwenda nchi ya ahadi. Lakini mfalme wa Misri mwenye cheo cha Farao alikataa hivyo Mungu alituma mapigo dhidi ya Misri ili Farao alazimishwe kukubali. Pigo la mwisho tena la kali mno lilikuwa kifo cha kila aliyezaliwa kama mtoto wa kiume wa kwanza katika Misri. Hapo Wanaisraeli waliambiwa kuchinja kondoo na kupaka damu milangoni kwao ili malaika akipita kuua watoto wa kwanza asiguse watoto wa Wanaisraeli. Baada ya pigo hili Farao alikubali Wanaisraeli watoke.

Tendo hili la kuwaweka mababu yao huru linakumbukwa na Wayahudi kote duniani katika siku zinazoanza Nisan 15.

Sherehe ya Pasaka

Sherehe ya Pasaka inaanza masaa ya jioni kabla ya siku yenyewe kwa sababu katika kalenda ya kiyahudi mwanzo wa siku si usiku manane wala macheo lakini wakati wa machweo jioni inayotangulia. Maandalizi ya sikukuu ni pamoja na kufanya usafi kabisa katika nyumba. Hakuna kitu kilichochachuka kinachobaki katika nyumba kufuatana na Kutoka 12:20, yaani kitu chochote chenye nafaka au unga wake ulioguswa na maji hata punje yake kama vile mkate, keki au spagetti. Tendo hili ni la kukumbuka jinsi Wanaisraeli walipaswa kukimbia Misri haraka bila muda wa kutengeneza mikate ya kawaida yaliyochachuka. Kwa hiyo wanawake wao walioka mikate yasiyochachuka ambayo yamekuwa chakula cha Pasaka hadi leo. Mikate hii huitwa "matze".

Familia na marifiki hukutana kwa chakula cha pekee wakizunguka meza ya Seder (seder = "utaratibu") yenye vyakula vya pekee. Kati ya vyakula hivi ni majani machungu yanayokumbusha uchungu wa utumwa, matunda ya kupondwa yenye rangi ya kahawia-nyekundu yanayokumbusha udongo wa matofali Wanaisraeli walipaswa kutengeneza, maji ya chumvi ya kukumbuka machozi huko Misri, mayai kama ishara ya matumaini, na vingine. Vyote huliwa katika utaratibu (=seder) maalumu pamoja na masomo na sala kutoka vitabu vya Haggada vinavyoshikwa na wote mezani.


Makala haya ni kwa mujibu wa wikipedia.org.

=================
Pasaka ni mnyama anayechinjwa kukumbuka kukombolewa Waisraeli Misri, siyo 'kufa' kwa Yesu

Ukweli wa Pasaka kama alivyofundisha Mungu
Kwa mujibu wa mafundisho ya Biblia, Pasaka ni mnyama ambaye wana wa Israeli waliamrishwa na Mungu wamchinje na wamle kwa kufuata utaratibu aliouelekeza Mungu na kwa lengo maalum. Maandiko yafuatayo yanathibitisha ukweli huu:
"Hapo ndipo Musa aliwaita wa Israeli, na kuwaambia, Nendeni, mkajitwalie wana kondoo kama jamaa zenu zilivyo, mkamchinje Pasaka". (Kutoka 12:21),
"Nawe umchinjie Pasaka BWANA, Mungu wako, katika kundi la kondoo na la ng'ombe, mahali atakapochagua BWANA apakalishe jina lake". (Kumbukumbu la Torati 16:2),
"Usimchinje Pasaka ndani ya malango yako yote akupayo BWANA, Mungu wako, ila mahali atakapochagua BWANA, Mungu wako, apakalishe jina lake, ndipo mtakapomchinja Pasaka jioni, katika machweo ya jua, kwa wakati kama uliotoka Misri". (Kumbukumbu la Torati 16:5-6).
Kulingana na maandiko hayo juu, tunaona hapa Biblia inafundisha wazi kuwa Pasaka ni kondoo au ng'ombe ambaye Mungu aliwaamuru wana wa Israeli wamchinje kisha wamle. Aidha, maandiko hayo yanaonyesha wazi pia kuwa amri hiyo (ya kuchinja na kumla Pasaka) haikuwahusu watu wa mataifa mengine isipokuwa Waisraeli peke yao.
Utaratibu aliouweka Mungu wa kumla Pasaka
Pamoja na wana wa Israeli kuamriwa na Mungu kumchinja Pasaka, Mungu pia aliwawekea utaratibu (sheria) wa kumla (Pasaka) kama tunavyosoma katika maandiko yafuatayo:
"BWANA akamwambia Musa na Haruni, Amri ya Pasaka ni hii; mtu mgeni asimle; lakini mtumishi wa mtu awaye yote aliyenunuliwa kwa fedha, ukiisha kumtahiri, ndipo hapo atamla Pasaka. Akaaye kwenu hali ya ugeni, na mtumishi aliyeajiriwa, wasimle Pasaka. Na aliwe ndani ya nyumba moja; usiichukue nje ya nyumba nyama yake yoyote; wala msivunje mfupa wake uwao wote. Na wafanye jambo hili mkutano wa Israeli wote. Na mgeni atakapoketi pamoja nawe, na kupenda kumfanyia BWANA Pasaka, waume wake wote na watahiriwe, ndipo hapo akaribie na kufanya Pasaka, naye atakuwa mfano mmoja na mtu aliyezaliwa katika nchi; lakini mtu yeyote asiyetahiriwa asimle. Sheria ni hiyo moja kwa mtu aliyezaliwa kwenu, na kwa mgeni akaaye kati yenu ugenini. Ndivyo walivyofanya wana wa Israeli wote; kama BWANA alivyowaagiza Musa na Haruni; ndivyo walivyofanya". (Kutoka 12:43-50)
"BWANA akanena na Musa, akamwambia, mtu wa kwenu, au vizazi vyenu, yeyote atakayekuwa na unajisi kwa ajili ya maiti, au akiwako mbali katika safari, na haya yote, ataishika Pasaka kwa BWANA; mwezi wa pili, siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, wataishika watamla pamoja na mikate isiyotiwa chachu na mboga za uchungu; wasisaze kitu chake chochote hata asubuhi, wala wasimvunje mfupa wake, kama hiyo sheria yote ya Pasaka ilivyo ndivyo watakavyoishika. Lakini mtu aliyesafi, wala hakuwa katika safari, naye amekosa kuishika Pasaka, mtu huyo atakataliwa mbali na watu wake; kwa sababu hakumtolea BWANA matoleo kwa wakati wake ulioamriwa, mtu huyo atachukua dhambi yake. Na kama mgeni akiketi kati yenu ugenini, naye ataka kuishika Pasaka kwa BWANA; kama hiyo sheria ya Pasaka ilivyo, na kama amri yake ilivyo, ndivyo atakavyofanya; mtakuwa na sheria moja, kwa huyo aliye mgeni, na kwa huyo aliyezaliwa katika nchi". (Hisabu 9:9-14).
Kwa kifupi, kama maandiko hayo yanavyoeleza, huo ndio ulikuwa utaratibu wa kumla Pasaka, ambao Mungu aliwawekea wana wa Israeli. Aidha, maandiko hayo nayo pia bado yanatuonyesha kuwa Pasaka ni mnyama ambaye Mungu aliwaamuru wana wa Israeli (peke yao) wamchinje kisha wamle.
Siku na muda aliouweka Mungu wa kuchinja na kumla Pasaka
Pamoja na Mungu kuwatajia wana wa Israeli watu wanaoruhusiwa kumla Pasaka (kama tulivyoona katika maandiko yaliyotangulia), Mungu pia aliwapangia siku na muda maalum wa kuchinja na kumla Pasaka, kama maandiko yafuatayo yanavyoeleza:
"Kisha BWANA akanena na Musa katika bara la Sinai, mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya kutoka kwao katika nchi ya Misri, akamwambia, Tena wana wa Israeli na washike sikukuu ya Pasaka kwa wakati wake ulioagizwa. Siku ya kumi na nne kwa mwezi huu, wakati wa jioni, mtaishika kwa wakati wake ulioagizwa; kwa amri zake zote, na kama hukumu zake zote zilivyo, ndivyo mtakavyoishika. Kisha Musa akawaambia wana wa Israeli kwamba waishike sikukuu ya Pasaka. Nao wakaishika Pasaka katika mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, katika bara ya Sinai, vile vile kama haya yote BWANA aliyomwagiza Musa, ndivyo walivyofanya wana wa Israeli". (Hesabu 9:1-5)
"Tena, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi, ni Pasaka ya BWANA". (Hesabu 28:16)
"Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi wakati wa jioni, ni Pasaka ya BWANA". (Mambo ya Walawi 23:5)
"Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume wa mwaka mmoja; mtamtwaa katika kondoo na mbuzi. Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na kusanyiko lote la mkutano wa Israeli watamchnija jioni". (Kutoka 12:5-6)
Kulingana na maandiko hayo juu, tunaona kwamba siku ya Pasaka ambayo Mungu aliwapangia wana wa Israeli kuishika ilikuwa ni kila ifikapo tarehe 14 mwezi wa kwanza wa mwaka wa kutoka kwao nchini Misri. Aidha, kama maandiko mengine ya Biblia yanavyofundisha (tazama Kumbukumbu la Torati 16:1) mwezi huo uliitwa "mwezi wa Abibu" ambao ulianza kuhesabiwa kabla hata Nabii Issa au Yesu (a.s.) hajazaliwa (B.C.). Ni wazi kuwa shuhuda hiyo peke yake inadhihirisha kuwa Pasaka kuwekwa tarehe 2 mwezi wa nne wa mwaka wa kuzaliwa Yesu (A.D.) kama wanavyofanya Wakristo leo, kwa kweli hiyo si katika mafundisho sahihi ya Mungu, bali ni uzushi mtupu uliobuniwa na wanaadamu!
Lengo sahihi la Mungu kuweka sikukuu ya Pasaka
Sambamba na Mungu kuwawekea wana wa Israeli utaratibu maalum wa jinsi ya kutekeleza amri yake ya kuchinja na kumla Pasaka, vile vile Mungu hakuacha kubainisha lengo hasa la kutoa amri hiyo kwa wana wa Israeli, kama maandiko yafuatayo yanavyobainisha hapa chini:
"Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie Pasaka BWANA, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku BWANA; Mungu wako, Nawe umchinjie Pasaka BWANA, Mungu wako, katika kundi la kondoo na la ng'ombe, mahali atakapochagua BWANA apakalishe jina lake. Usimle pamoja na mikate iliyotiwa chachu; siku saba utakula naye mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso; kwa maana ulitoka nchi ya Misri kwa haraka; ili upate kukumbuka siku uliyotoka nchi ya Misri, siku zote za maisha yako". (Kumbukumbu la Torati 16:1-3).
Kufuatana na maandiko hayo juu, tunaona kuwa lengo la Mungu kuwawekea wana wa Israeli sikukuu hiyo ya Pasaka, ilikuwa ni kwa ajili ya kukumbuka siku aliyowakomboa kuwatoa nchini Misri chini ya utawala ya Farao (Firauni). Ambapo maandiko ya Biblia yamearifu kuwa wana wa Israeli walikaa nchini Misri katika hali ya utumwa kwa muda usiopungua miaka 430 (tazama Kutoka 12:40-42)).
Aidha, maandiko hayo yanaonyesha lengo lingine la Mungu kuwawekea wana wa Israeli sikukuu hiyo (Pasaka) ilikuwa kama desturi yake kujenga uhusiano mzuri baina yake na wanaadamu endapo watatii amri zake.
Makala haya yameandaliwa na Muhibu Said

Newer Post Older Post