LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

UPENDO NKONE ACHUMBIWA

Ni miaka tisa (9) sasa ya ujane, lakini kwa Mungu hatukati tamaa, hatimaye mwimbaji wa muziki wa Injili Bongo, Upendo Nkone, amepata mwenza wa maisha ambaye ameanza na hatua ya mwanzo ya kumchumbia kabla ya kumbeba jumla, Risasi linabeba mabango ya nderemo.
Akistorisha na gazeti hili jijini Dar es Salaam juzikati, Upendo aliweka kweupe kwamba, amekuwa katika maombi ya mnyororo akimuomba Mungu ampe mume mwema ambaye atafanyika faraja katika maisha yake ikiwa ni pamoja na kupata heshima ya kuitwa mama fulani katika jamii inayomuzunguka.
“Namshukuru Mungu amejibu maombi yangu, tayari nimempata mwenza wa maisha ambaye ameanza hatua za mwanzo za kunichumbia, naye atafanyika faraja kubwa kwangu kwani nilidharaulika katika jamii inayonizunguka,” alisema Upendo kwa masikitiko makubwa.
Mtumishi huyo wa Mungu aliendelea kumwaga ‘data’ kwamba, kwa kipindi chote hiyo cha ujane amekumbana na misukosuko mingi ikiwa ni pamoja na kutokewa na wanaume wenye fedha zao ambao walionekana kuvutiwa naye, lakini Jehova alimuzuia na kuachana nao mpaka alimpompa wa kufanana naye.
“Nimeishi katika mazingira magumu ya ujane tangu mwaka 2002 nilipoondokewa na mzazi mwezangu, wanaume wengi walijitokeza wakitaka kunioa, moyo wangu haukuwa na amani nao licha ya kuwa na uwezo mkubwa wa kifedha, ashukuriwe Mungu amenipa wa kufanana nami ambaye nitamuweka hadharani siku si nyingi,” alisema Upendo.
Aidha, staa huyo anayetesa na ngoma yake ya ‘Unitetee Mokozi Wangu’ alisema kwamba, suala la upweke, kukosa uhuru wakati wa usiku anapotoka kwenye huduma, ama kutembea usiku peke yake, kukaa na simanzi muda mwingi vimechangia kwa kiasi kikubwa kutulia katika magoti kumsihi Mungu ampe mbadala na mzazi mwenza.
Akielezea sababu za kutomuweka wazi kwa sasa mumewe mtarajiwa, Upendo alisema kuwa, anachoogopa ni wadaku ambao wanaweza kutibua na kumfanya aendelee kusota katika hali ya ujane.
Kondoo huyo wa Mungu alimalizia kwa kuwataka wajane wenzake kutulia katika uwepo wa Mungu ili wasiangukie katika dhambi ya uasherati kutokana na kuzungukwa na vishawishi vya kila namna, ambapo yeye binafsi alikuwa na mpango wa kuandaa tafrija fupi ya kujipongeza kuishi maisha matakatifu kwa muda wote huo.

Newer Post Older Post