LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

Christina Shusho akanyaga sikendo


Mkali wa Muziki wa Injili Bongo, Christina Shusho amepangua vikali madai yanayovumishwa kila kona ya jijini la Dar kuwa, amekuwa na kijitabia cha kutapanya fedha zake vibaya kwa kufanya matanuzi ambayo kwa hadhi yake hapaswi kuyatenda.
Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni jijini Dar es Salaam, Shusho alisema kuwa, anashangazwa na uvumi huo ambao hauna ukweli wowote bali una lengo la kuinajisi huduma yake ili aeleweke vibaya katika jamii.
“Si kweli kwamba mimi nafanya matanuzi kwa kutumia fedha kama watu wanavyodai, bali naona watu wameamua kunichafua kwa maneno ya uzushi ili jamii inichukie ikiwa sambamba na kuinajisi huduma yangu,” alisema Shusho ambaye ni miongoni mwa waimbaji wachache wa muziki huo ambao wamekuwa wakihesabika kuwa ‘wasafi’.
Mbali na matumizi mabaya ya pesa, msanii huyo anadaiwa kulala kwenye hoteli za nyota 5 punde anaporejea jijini usiku akitoka kufanya shoo zake mikoani.
Wadaku hao walisema kuwa, Mtumishi huyo wa Mungu amekuwa akifanya hivyo kutokana na uwezo mkubwa wa kifedha alionao bila kuangalia kama kuna watu ambao wanahitaji msaada kutokana na maisha magumu wanayoishi hasa wajane na yatima.
Akipangua skendo moja baada ya nyingine, Shusho alikiri kwanza kuwa na safari za kwenda kununua nguo zake nje ya nchi akisema kwa sababu ana duka la nguo Kariakoo.
Aisha, alisema kuwa, yeye ni mwanamitindo hivyo anapokwenda Marekani, Uingereza au China hununyua vitambaa ambavyo vikishonwa na kuvaa huonekana amenunua nguo za gharama kubwa.
“Mimi ni mtu ninayetumika madhabahuni, natakiwa nionekane nadhifu muda wote, na kweli nimekuwa nikisafiri kwenda Ulaya kununua bidhaa za dukani kwangu, na nikiwa huko huwa nanunua kitambaa kimoja kimoja, nikija kushona nguo na kuvaa zinaonekana nzuri na za gharama ya juu na baadhi ya watu hutafsiri kwamba, natumia vibaya fedha zangu,” alisema Shusho.
Akifafanua kuhusu suala la kulala hoteli za gharama nchini anaporeja Dar usiku toka kwenye shoo, Shusho alisema kuwa, jambo hilo halina ukweli wowote kwa sababu ana mapenzi na familia yake hivyo hawezi kufanya kitendo kama hicho.
Mwimbaji huyo alimaliza kwa kusema kuwa, yote hayo anamwachia Mungu yeye ndiye anayejua ukweli wa maisha yake, na masuala hayo anayapeleka kiroho zaidi kuliko kimwili kwani yanaweza kuujeruhi moyo wake.
“Namwachia Mungu masuala hayo, yeye ndiye anayefahamu ukweli wa maisha yangu kwa maana Biblia inasema; Kushinda kwetu si kwa damu na nyama bali ni katika Ulimwengu wa roho, Jehova atalidhibitisha jambo hili kama lipo, na kama halipo wanaovumisha maneno hayo atawashughulikia,” alisema Shusho.

Newer Post Older Post

One Response to “Christina Shusho akanyaga sikendo”

Boaz Nundu CPA(K) said...

You people of Dar(Tz) are strange . This lady is your sister,engaged in winning souls for our Lord Jesus Christ.Why use the media to box her?What is the gain in trampling on her ? Ikindly beg you to lift this lady up for the sake of the gospel-Boaz Nundu,Nairobi -Kenya (boaznund@yahoo.com)