LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

TAMASHA KUBWA LA INJILI LAANDALIWA MBEYA



Tamasha kubwa la muziki wa  injili limeandaliwa na mwimbaji  wa nyimbo za injili nchini Mwinjilisti Kabula George  na litafanyika katika kanisa la Moravian Usharika wa Yerusalem Air Poirt Mbeya mjini Julai 21 mwaka huu na litaenda sambamba na kuizindua kwa mara nyingi DVD yake ya albamu ya Nitang’ara Tu.
 Akizungumza na Tanzania Gospel Music leo jijini Dar es Salaam, Mwinjisti Kabula alisema kuwa ameamua kuaandaa tamasha hilo kutokana  na wakazi wa jiji hilo kuomba aandae tamasha hilo kutokana na kuzipenda nyimbo zake ambazo zimekuwa zikiwagusa kila wanapozisikiliza redioni.
“Nimeandaa tamasha hilo mkoani  Mbeya baada ya kupokea maombi ya wakazi  wengi  wa Nyanda za Juu Kusini nami nimeona nikubali ombi lao na taratibu zote kwa ajili ya tamasha hilo yanaendelea hivyo naamini wakazi wa mkoa huo watapata kile wanachokitaka,” alisema Mwinjilisti Kabula.
Mwimbaji huyo alisema kuwa tamasha hilo litakuwa na waimbaji wengi kutoka mikoa mbalimbali kama Njombe, Dar es Salaam na wenyeji Mbeya na kuahidi kuacha histoaria nyanda hizo.
“Litakuwa tamasha la kipekee kufanyika katika mkoa huo kwani litawakutanisha waimbaji nyota kutoka katika mikoa mitatu ambayo ni Njombe, Dar es Salaam na wenyeji Mbeya hivyo si siku ya kukosa,” alisema Mwinjilisti Kabula.
Mwinjilisti Kabula alisema pia kuwa siku hiyo kwa mara ya kwanza ndipo ataziuza DVD zake kwa mashabiki wote watakaofika katika uzinduzi huo na anaamini kila mmoja ataondoka na nakala yake halisi.

Newer Post Older Post