LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

Anna Clara Masala: Muziki wa Injili ni kazi ya Mungu, si umaarufu



Leo katika TGM nakuletea muimbaji wa muziki wa  Injili, Anna Masala ambaye ni miongoni mwa waimbaji wa muziki huo nchini Tanzania ambaye ameamua kuimba nyimbo za kumsifu Mungu tangu mwaka 1997 mara baada ya kupata nafasi ya kumpokea Bwana Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake.
“Pamoja na ukweli huo lakini nikwambie jambo moja ambalo mimi ninaliona kuwa si sahihi nalo ni ushirikiano mdogo  na kukosekana upendo wa dhati miongoni mwetu sisi waimbaji wa muziki wa Injili,” anasema Anna.
Akizungumzia juu ya  mwanzo wa huduma yake, Anna  anasema kwamba  kazi ya uimbaji alianza kuifanya akiwa muimbaji wa kwaya ya kanisani alipokuwa anaabudu, (Tanzania Assemblies of God -TAG-Kinondoni) ambapo kupitia muziki huo, Mungu ameweza kumsimamia kwenye masuala mengi ya kimaendeleo.
Miongoni mwa mambo ambayo anaamini kuwa yametokana na matunda ya kufanya kazi ya kuhubiri Injili kwa njia ya nyimbo,  ni pamoja na kupata kazi za kucheza filamu tatu ambazo ni Hero of Church, Kiapo na Danger Zone jambo analoamini kuwa ni kutokana na rehema za Mungu tu.
 “Haya kwangu nayaona kuwa ni mafanikio makubwa, lakini haikuwa ni safari nyepesi kwa sababu nilikutana na vikwazo vingi katika maisha yangu, hii si mimi pekee bali waimbaji wengi hukabiliana na mambo haya.
“Pamoja na  hayo, pia muziki huu umekuwa ukitumika kwa ajili ya kubadilisha tabia na miondoko ya wanajamii na kumtangaza Mungu, lakini cha kushangaza wapo baadhi ya waimbaji hawapendani, jambo ambalo ni baya kwa mustakabali wa huduma hii,” anaongeza muimbaji huyo ambaye bado hajapata jina kubwa ikilingansihwa na waimbaji wengine waliopo juu hivi sasa kama Rose Mhando, Bahati Bukuku na Upendo Nkone.
Akielezea ushirikiano uliokuwepo baina ya  waimbaji chipukizi, anasema kuwa  kila wakati wamekuwa wakipeana moyo na kuamini kuwa kufanya muziki wa Injili si kwa ajili ya kutafuta fedha, au umaarufu bali ni kazi ya wito ili kuwaokoa watu wa Mungu na matatizo ya kidunia.
“Japokuwa ni kazi ya Mungu lakini kuna tatizo lingine kubwa nalo ni usumbufu kwenye studio wakati tukijiandaa kurekodi. Hii ni kutokana na ukweli kwamba studio hizihizi ndizo zinazotumika kurekodi nyimbo za kidunia,” anaongeza mwanadada huyo aliyejikita vilivyo kwenye imani ya kilolole.
Aneleza kuwa studio nyingi za kidunia zinakuwa na matatizo ya kuiba kazi za waimbaji na kuziuza kinyemela huku akikiri kuwa hata yeye alitokewa na jambo hilo.
 “Nimalizie kwa kusema kuwa huduma ya uimbaji wa nyimbo za Injili inagusa zaidi kumtumikia Mungu na siyo kujulikana kama baadhi ya watu wanavyodhani, na wakati huo huo  niwape moyo watumishi wa Mungu kutokana na kujituma kwao kwenye huduma hii,” anamaliza Anna.





Newer Post Older Post

One Response to “Anna Clara Masala: Muziki wa Injili ni kazi ya Mungu, si umaarufu”

Anonymous said...

Watu wengi wanachanganya kuokoka na kuimba nyimbo za Injili. Inatakiwa unachokiimba kiendane na matendo yako. Nakufahamu vizuri huna ulokole wa aina yoyote, badilika na mungu atakusaidia.