LULU, PACHA WA DOTNATA NDANI YA MBEYA AGOSTI 4,2013

WASANII WA FILAMU NCHINI ELIZABETH MICHAEL (LULU) NA PACHA WA DOTNA NI MIONGONI MWA WAGENI WATAKAOHUDHURIA TAMASHA LA KUITAMBULIA ALBAM YA NITANG’ARA TU YA MWINJILISTI KABULA GEORGE UTAKAOFANYIKA KATIKA MKOA WA MBEYA TAREHE 4 MWEZI WA 8, 2013. SEHEMU AMBAPO LITAFANYIKA TAMASHA HILO ITATANGAZWA HIVI KARIBUNI. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0755 240136/0712001880.

JIPATIE SOFA SAFI KWA KOMBA SOFA SHOORM MKOANI MBEYA

KOMBA SOFA SHOORM (YESU NDIYE) NI WATENGENEZAJI WA SOFA ZA KISASA NA KUZIUZA KWA GHARA NAFUU SANA. WAPO MBEYA STRIRED JIRANI NA KANISA LA HIJA MWANJELWA JIRANI NA KANISA KUBWA WA ROMA. WASILIANA NAO KWA SIMU NAMBA 0754553467 AU 0655 553467. NYOTE MNAKARIBISHWA.

ECK PRODUCTION STUDIO YA KISASA NA KIMBILIO LA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI TANZANIA.



IPO MWEMBECHAI JIJINI DAR ES SALAAM, TANZANIA WAIMBAJI KAMA ROSE MUHANDO, HABATI BUKUKU, BONY MWAITEGE,UPENDO NKONE, JANGALA SON, MWANSASU NA WENGINE WENGI WAMEREKODIA KATIKA STUDIO HIYO. WASILIANA NAO KWA NAMBA +255 656 388 404

REDIO USHINDI FM KIPENZI CHA WATU WENGI NYANDA ZA JUU KUSINI

Gwajima

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ametoa mpya kwa kutahadharisha kuhusu tiba ya kikombe cha Mchungaji Ambilikile Masapile wa Samunge, Loliondo kwa kusema kuwa endapo dawa hiyo anayoitoa inaponyesha watu asibughudhiwe wala asipigwe vita.

Gwajima alitoa tahadhari hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita kanisani kwake jijini Dar es Salaam katika Viwanja vya Tanganyika Pakers, Kawe alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa gazeti hili juu ya msimamo wake juu tiba anayoyatoa mchungaji Masapile maarufu kwa jina la Babu.
Alisema kwamba hajajua kama dawa hiyo inaponyesha watu au laa na kueleza kuwa, kama wagonjwa wanaoitumia wanapona ni jambo zuri, hivyo hakuna sababu ya kubughudhiwa bali apewe ushirikiano ili aendelee kuwasaidia wagonjwa.
“Hao watu wanaompiga vita Masapile ina maana wameshindwa kuwasaidia wagonjwa na ndiyo maana wanakimbiwa na kubakia kulalamika huku wakiponda huduma anayoitoa mchungaji huyo. Wagonjwa ni wajanja sana, wanaangalia ni wapi wanaweza kupata uponyaji,” alisema Gwajima.
Aliongeza kusema kuwa, kunywa dawa ya miti si dhambi kwani hata vidonge vinavyotumika kutibu magonjwa mbalimbali vinatokana na mimea isipokuwa huwa vinatengenezwa kiwandani, hivyo haoni tatizo kwa Masapile kutumia uponyaji wa mizizi anayodai kuoteshwa na Mungu.

Newer Post Older Post

2 Responses to “Gwajima”

asigwa james said...

ni suala zuri kwa mchungaji au mtumishi mmoja kutambua kazi anayofanya mtumishi mwingine hata kama ametoka kitofauti.. namuunga mkono gwajima kwani ata yesu alishaletewa kes ya namna hii kuusu wanafunzi wa yohana kufanya kazi kama za yesu yesu akawaambia "WAACHENI WAKO ASIYEKUWA KINYUME CHETU YUKO UPANDE WETU " hivyo sioni ugumu wa jambo hili kwa sbs tu masapile si mlokole

asigwa james said...

ni suala zuri kwa mchungaji au mtumishi mmoja kutambua kazi anayofanya mtumishi mwingine hata kama ametoka kitofauti.. namuunga mkono gwajima kwani ata yesu alishaletewa kes ya namna hii kuusu wanafunzi wa yohana kufanya kazi kama za yesu yesu akawaambia "WAACHENI WAKO ASIYEKUWA KINYUME CHETU YUKO UPANDE WETU " hivyo sioni ugumu wa jambo hili kwa sbs tu masapile si mlokole